TMA yatoa tahadhari ya kimbunga Dikeledi

 

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) leo Jumanne Januari 14, 2025 imetoa taarifa ya uwepo wa Kimbunga Dikeledi katika Bahari ya Hindi mwambao wa pwani ya Msumbiji.

Taarifa ya mamlaka hiyo imeeleza kuwa mifumo ya hali ya hewa inaonesha kimbunga hicho kwa sasa kipo mwambao wa pwani ya Msumbiji na kinatarajiwa kurejea katika Rasi ya Msumbiji leo alasiri huku ikibainisha kuwa kimbunga hicho hakiashirii uwezekano wa kusababisha athari za moja kwa moja hapa nchini.

Hata hivyo, kutokana na ukaribu wa maeneo ambayo Kimbunga Dikeledi kipo sambamba na maeneo ya kusini mwa nchi yetu, upo uwezekano mdogo wa matukio ya vipindi vifupi vya mvua kubwa katika maeneo ya pwani ya kusini hususan katika mikoa ya Lindi na Mtwara kwa siku ya leo Januari 14, 2025, imeeleza taarifa hiyo.

Chapisha Maoni

0 Maoni