Rais Samia Suluhu Hassan ameipongeza Zanzibar Heroes kwa
kufanikiwa kufika hatua ya fainali ya Kombe la Mapinduzi na kuahidi katika
mchezo wa fainali kutakuwa na zawadi ya fedha za Goli la Mama.
Rais Samia ametoa pongezi hizo kupitia akaunti yake ya
mtandao wa Instagram, kwa kuandika yafuatayo:-
Ninaipongeza Zanzibar Heroes kwa kufanikiwa kufika hatua
ya fainali ya Mashindano ya Kombe la Mapinduzi. Mmejitoa, mmejituma na sote
tunajivunia safari yenu hadi sasa.
Mchezo huu wa fainali ni nafasi ya kipekee kwenu kuandika
historia, nasi tuko nyuma yenu kuwaunga mkono.
Ninawatakia kila la kheri, na ninawaahidi katika mchezo
huu wa fainali Goli la Mama litakuwepo.
0 Maoni