Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Mwinyi ameialika timu ya Taifa ya Zanzibar, Zanzibar Heroes Ikulu kwa
chakula cha mchana siku ya Jumatano
tarehe 15 Januari 2025.
Rais Dk. Mwinyi ametoa mwaliko huo Uwanja wa Gombani Pemba
baada ya timu hiyo kufanikiwa kulitwaa Kombe la Michuano ya Mapinduzi 2025.
Zanzibar Heroes imeifunga
timu ya Taifa ya Burkinafaso kwa magoli
2-1 katika mchezo mkali wa fainali uliochezwa uwanja wa Gombani Mgeni Rasmi akiwa Rais Dk. Mwinyi ambae alikabidhi kombe kwa bingwa wa michuano hiyo
Zanzibar Heroes.
Zanzibar Heroes ilitinga fainali badaa ya kuilaza timu ya taifa ya Kenya Harambe Stars kwa goli 1-0. Licha ya kombe la ubingwa timu hiyo pia imejinyakulia kitita cha Shilingi Milioni 100.



0 Maoni