Raia wadhibitiwa kuchota mafuta ajali ya lori la mafuta

 

Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoani Morogoro kwa kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama wamefanikiwa kudhibiti kundi la watu waliofurika kuchota mafuta baada ya Lori lenye usajili namba T 257 EAU lililokuwa likisafiri kutoka Dar es salaam kuelekea njombe kuanguka maeneo ya mzambarauni Manispaa ya Morogoro leo Januari 15, 2025

Mrakibu Msaidizi (ASF) Daniel Ibrahim myalla wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoani humo akizungumza na waandishi wa Habari amèwataka wananchi kuacha kukimbilia kuchota mafuta katika magari pale yanapopata ajali kwani inaweza kusababisha mlipuko na hatimaye kusababisha vifo.

Chapisha Maoni

0 Maoni