Polisi wampata mtoto aliyeibwa pamoja na gari

 

Polisi mkoani Pwani wamefanikiwa kumpata mtoto mwenye umri wa miezi sita aliyechukuliwa na watu wasiojulikana, baada ya kuvamia nyumba ya Melksedek Mrema na mkewe Joan Gabriel, ambao nao wakati wa tukio hilo walitupwa kwenye mashimo ya choo, kabla ya watuhumiwa kuondoka na mtoto huyo pamoja na gari.

Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Salim Morcane amesema majira ya saa 9.00 usiku wa kuamkia jana Januari 24, 2025, katika eneo la Kimalamisale, Mtaa wa Serengeti B uliopo Kata ya Dutumi, Kibaha vijijini waliwakamata wanaume watatu na mwanamke mmoja aliyekutwa na mtoto huyo wa kike na gari Toyota IST.

Kamanda Morcane ameeleza kuwa baada ya kumpata mtoto, walimpeleka katika Hospitali ya Tumbi kwa uchunguzi Zaidi, kisha atakabidhiwa kwa wazazi lakini kwa sasa yupo sehemu salama zaidi.

Chapisha Maoni

0 Maoni