Mtu mmoja apatikana na maambukizi ya Marburg Kagera

 

Mtu mmoja ambaye alikuwa akigua ugonjwa wa Marburg amegunduliwa nchini Tanzania.

Akizungumza katika mkutano na Katibu Mkuu wa Shirika la Afya Duniani WHO Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema kwamba serikiali yake ilichukua hatua kufuatia uvumi uliokuwa ukiendelea katika eneo la Kagera.

Amesema kwamba sampuli zilizochukuliwa katika hospitali moja mjini Kagera na kuthibitishwa mjini Dar es Salaam zilimtambua mtu huyo aliyekuwa na virusi vya maradhi hayo.

Hatahivyo sampuli za washukiwa wengine wa maradhi hayo hazikupatikana na ugonjwa huo hatari.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa WHO Dkt. Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema wamedoa dola za Marekani milioni 3 ili kusaidia Tanzania kudhibiti maradhi hayo, ikiwa ni pamoja na dola 50,000 ambazo shirika hilo lilitoa ili kusaidia katika uchunguzi.

Dkt.  Adhanom amesema kufikia sasa hakuna chanjo wala tiba iliothibitishwa kukabiliana na virusi vya Marburg licha ya kwamba kuna mipango ya kuafikia hayo.

Dkt.  Adhanom ameongezea kuwa milipuko inaweza kudhibtiwa kupitia mikakati ya kuzuia maambukizi na kuokoa maisha kama ilivyofanya Tanzania.

Chapisha Maoni

0 Maoni