Maelfu wakimbia mapigano ya Jeshi na waasi wa M23

 

Maelfu ya raia wameripotiwa kukimbia mapigano kati ya jeshi la nchi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na waasi wa kundi la M23 mashariki mwa nchi hiyo.

Jeshi na washirika wake wamekuwa wakipambana kuukomboa mji wa Masisi ambao hivi karibuni uliangukia mikononi mwa waasi hao.

Mashirika ya misaada ya kibinadamu yameonya kuwa raia wako katika hatari kubwa huku silaha nzito zikitumiwa katika maeneo ya makazi ya raia vitongojini.

Waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda wanaonekana kudhamiria kupanua sehemu wanayodhibiti katika eneo mashariki mwa Kongo lenye utajiri wa madini.

Chapisha Maoni

0 Maoni