Akamatwa kwa kusambaza picha za utupu

 

Jeshi la Polisi mkoani Pwani linamshikilia mtuhumiwa mmoja ambaye jina lake limehifadhiwa kwa tuhuma za kukutwa na picha mjongeo za utupu zenye maudhui machafu kimaadili kinyume na Sheria pamoja na kifaa cha kielektroniki ambacho alikuwa akitumia kusambaza picha hizo chafu.

Akizungumza na vyombo vya habari Kamanda wa Polisi mkoani Pwani Salim Moracase amesema walimnasa mtu huyo baada ya kupokea taarifa kutoka kwa uongozi wa Shule ya Baobab, iliyopo Bagamoyo mkoani Pwani, kuwapo kwa watu waliotengeneza picha walizoziuganisha na baadhi ya majengo ya shule ili kuaminisha umma kuwa vitendo hivyo vinafanyika shuleni hapo.

Jeshi la polisi limefanya uchunguzi limefanikiwa kumkamata mtu mmoja ambaye uchunguzi wa kitaalamu ulisaidia kumfikia na kumkuta na picha hizo na kifaa ambacho alikuwa akitumia kusambaza picha hizo chafu, amesema Kamanda Moracase.

Aidha, Kamanda Moracase amesema polisi bado wanaendelea kuwasaka watu wengine waliohusika katika kutengenezea na kusambaza picha hizo.

Jeshi hilo limetoa onyo kwa watu wenye tabia kama hizo za kutengengeneza picha kama hizo kwa malengo ya kuchafua wengine au taasisi kwani mkono wa sheria lazima utawafikia.

Chapisha Maoni

0 Maoni