Waziri Gwajima amlilia Graison, ataka ulinzi kwa watoto

 

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalumu, Dkt. Dorothy Gwajima ametoa pole kwa wazazi wa mtoto Graison Kenyenye aliyeuawa na watu wasiojulikana, na kuwataka wazazi na walezi kuimarisha ulinzi na usalama wa watoto.

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari aliyoitoa leo Desemba 27, 2024, Dk Gwajima amesema wizara yake imepokea kwa taarifa hizo za masikitiko kwa simanzi kubwa kutokana na mtoto huyo kukatishwa uhai wakati ndiyo kwanza alikuwa anaanza safari ya ndoto za maisha yake.

Tukio hilo limetokea Ilazo Extension jijini Dodoma Desemba 25, 2024, wakati mfanyabiashara Zainab Shaban maarufu Jojo alipomuacha mtoto huyo nyumbani kwa rafiki yake wa kiume ambaye ni Ofisa Uvuvi Mtera, Hamis Mpeta.

Taarifa ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, George Katabazi ilisema tukio  hilo limetokea Desemba 25, 2024 saa 1.00 asubuhi ambapo Mpeta akiwa na mama wa mtoto Zainab walibaini mtoto huyo kuuawa baada ya kurejea kutoka matembezini.

Kamanda Katabazi ameeleza kuwa walimkuta mtoto huyo akiwa ameuawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani na shingoni amekatwa na kitu chenje nja kali, na kuongeza kwamba mama wa mtoto alimwacha mtoto huyo chini ya uangalizi dereva bodaboda anayejulikana kwa jina la Kelvin Gilbert.

Chapisha Maoni

0 Maoni