Chama cha
ACT Wazalendo kimedai kuwa Mwenyekiti wake wa Ngome ya Vijana Abdul Nondo
ametekwa leo asubuhi na watu wasiojulikana alipowasili Jijini Dar es Salaam
akitokea mkoani Kigoma.
Nondo
alikuwa sehemu ya viongozi wa kitaifa wa chama hicho walioongoza kampeni za
uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwenye mikoa ya magharibi mwa Tanzania.
Taarifa
iliyotolewa leo na Naibu Katibu wa Haki za Binadamu na Vyombo vya Uwakilishi wa
Wananchi ACT Wazalendo Mbarala Maharagande imesema Nondo aliwasili stendi
Magufuli iliyopo Mbezi kwa usafiri wa basi la Saratoga lenye namba za usajili T
221 DKB.
Taarifa hiyo
imesema mashuhuda wa tukio hilo wamedai kulikuwa na purukushani katika utekaji
wa Nondo hali iliyosababisha begi lake dogo la nguo na pingu iliyobebwa na
mmoja wa watekaji kudondoka.
Chama cha
ACT Wazalendo kimelitaka Jeshi la Polisi kufuatilia tukio hilo ili kufanikisha
kupatikana kwa Nondo anapatikana akiwa salama.
0 Maoni