Wanavijini wamshukuru Rais Samia kwa gari la wagonjwa

 

Wanavijiji wa Kata ya Bugwema wamejawa na furaha tele baada ya Kituo cha Afya cha kata hiyo kupokea gari jipya la wagonjwa (Ambulance) lililotolewa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Wanavijiji hao kutoka Kata hiyo yenye vijiji vinne (Bugwema, Kinyang'erere, Masinono na Muhoji) wamemshukuru sana Mhe Rais Samia kwa kuwapatia gari jipya la wagonjwa (Ambulance).

Katika hafla ya kupokea gari hilo jana iliyohudhuriwa na Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini Prof. Sospeter Muhongo, wanavijiji hao wamesema kuwa gari hilo kwao ni zawadi ya pekee kutoka kwa Rais, “kwetu sisi tunaiona kama zawadi ya Krismasi.”

Wakiongea kwa nyakati tofauti wanakijiji hao wamesema kuwa gari hilo litawasaidia mno katika kuwapeleka wagonjwa ambao wanahitaji matibabu ambayo yameshindikana katika kituo hicho.

Kutokana na furaha waliokuwa nayo ya kutatuliwa kero ya kukosa gari la wagonjwa wanavijiji hao wameahidi kumpatia Mhe Rais wetu kura zote za Kata hiyo kwenye uchaguzi mkuu wa mwakani (2025).

Kwa upande wake Prof. Muhongo amemshukuru sana Mhe. Rais Samia, na kumpongeza kwa kuendelea kuwatumikia Watanzania kwa dhati katika kuwaletea maendeleo kwenye sekta mbalimbali zikiwamo za afya na elimu.


Chapisha Maoni

0 Maoni