Nchi ya Ukraine imesema imemuua Luteni Jenerali wa Urusi Igor Kirillov, ambaye amekufa kwenye tukio la mlipuko leo Jumanne Jijini Moscow.
Lt Jen. Igor Kirillov alikuwa katika eneo la kuingilia
nyumbani kwake wakati bomu lililofichwa kwenye pikipiki ya umeme lilipomlipukia.
Vyanzo kutoka kwenye taasisi ya usalama wa taifa wa
Ukraine, vimeliambia shirika la habari la BBC kuwa Kirillov alikuwa kwenye
mpango wa kushambuliwa.
Hapo jana Jumatatu, Kirillov alifunguliwa mashtaka Jijini
Kyiv kwa matumizi ya silaha za kemikali zilizopigwa marufuku.
Kirillov alishawekewa vikwazo na UK pamoja na mataifa
mengine kwa uhusika wake wa Urusi kutumia silaha za kemikali.
0 Maoni