Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema kuwa Tanzania itaingia tena kwenye ushindani wa kuwania nafasi ya Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) kanda ya Afrika, baada ya kumpoteza Mkurugenzi Mteule wa shirika hilo marehemu Dkt. Faustine Engelbert Ndugulile.
Rais Samia
ametoa kauli hiyo leo Desemba 2, 2024 Jijin Dar es Salaam, katika hotuba yake
fupi aliyoitoa wakati wa kuaga mwili wa Mkurugenzi Mteule wa Shirika la Afya
Duniani (WHO) Marehemu Dkt. Faustine Engelbert Ndugulile, katika viwanja vya
Karimjee.
“Lakini
niseme Dkt. Faustine katika safari yake hii ya mwisho ameweka heshima kubwa kwa
nchi yetu kwa kupata nafasi ile, naniseme kwamba Mungu amechukua amana yake
lakini kwetu sisi ni kwenda, tutawania tena nafasi ile,” alisema Rais Samia na
kuongeza, “Tutatafuta Mtanzania mwenye sifa zinazoweza kushindana na ulimwengu
tutaingia tena na tutaweka nguvu ileile ili kuweka heshima ya nchi yetu.”
Awali Mchungaji
Josephat Gwajima amemzungumzia aliyekuwa mbunge wa Kigamboni, Dk Faustine
Ndugulile, akisisitiza umuhimu wa kuelewa tafsiri sahihi ya maisha na wajibu wa
kila mtu duniani.
Akizungumza
kwa niaba ya wabunge wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mchungaji Gwajima amesema, “Ipo
sababu ya kupata tafsiri sahihi ya umuhimu wa maisha na maisha ni nini. Janga
si kifo; mtu mmoja alipata kusema janga ni kuwa hai wakati wengine wanakufa na
wewe hujui kwa nini uko hai.”
Dkt. Gwajima
amesema kuwa kila mtu amepewa misheni tofauti na Mungu, ikiwemo ya kisiasa,
kiuchumi, au kiroho, ambayo inapaswa kutimizwa kwa wakati.


0 Maoni