Shirika la
Reli Tanzania (TRC) limeongeza safari za treni kuelekea sikukuu za mwisho wa
mwaka kwa safari za kuelekea mikoa ya Tanga, Kilimanjaro na Arusha na kusema
kuwa hakutakuwa na ongezeko la nauli.
Taarifa ya Mkuu
wa Kitengo cha Uhusiano TRC Fredy Mwanjala imesema kuwa siku ya Jumatano itaongezeka
kujumuisha siku za Jumatatu na Ijumaa hivyo kufanya jumla ya safari tatu kwa
juma kuelekea mikoa hiyo.
Pia, kila
siku ya Jumatano ya juma Desemba 09, mwaka huu mpaka mwanzoni mwa Januari 2025,
TRC itapeleka mabehewa 18 yatakayobeba abiria zaidi ya 1,000 kwa wakati mmoja
kulekea katika mikoa hiyo.
Katika
taarifa yake hiyo TRC imesema ongezeko hilo ni hatua mahususi ya kukabiliana na
ongezeko la abiria katika kipindi hiki hususan kuelekea mikoa ya Kaskazini
Mashariki mwa Tanzania.
0 Maoni