Mabalozi waendelea kukwea Mlima Kilimanjaro

 

Safari ya mabalozi kupanda Mlima Kilimanjaro, hatimaye imesalia muda wa saa 96 kukifikia kilele kirefu zaidi barani Afrika cha Uhuru chenye urefu wa mita 5895 kutoka usawa wa bahari.

Safari ya siku sita ya kuelekea kilele cha Uhuru ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 63 ya Uhuru wa Tanganyika imeingia siku ya pili baada ya mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania nchi za nje kuendelea kupunguza vituo 2 na kubakiwa na vituo 3 kati ya vituo 5 hadi kileleni.

Safari ya kuukwea mlima huo huchukua takribani saa 144 ikiwa ni sawa na siku 6, lakini hadi jana jioni, waheshimiwa mabalozi hao walikuwa wamebakiza saa 96 kukifikia kilele hicho.

Mabalozi walioanza safari ya kuelekea katika kilele hicho kirefu kuliko vyote barani Afrika kupitia lango la Marangu ni pamoja na Mhe. Balozi Gelasius Byakanwa (​Burundi), Mhe. Balozi Prof. Adelardus Kilangi​ (​Brasilia) na Mhe. Balozi (IGP Mstaafu) Simon Sirro​ (​Zimbabwe).

Wengine ni Mhe. Balozi Saidi H. Massoro​ (Kuwait), Mhe. Balozi Innocent Shiyo​ (Ethiopia), Mhe. Balozi Dkt. Mahadhi J. Maalim​ (​Malaysia), Mhe. Balozi Habibu A. Mohamed​ (Qatar), Mhe. Balozi Baraka Luvanda (​Japan) na Mhe. Balozi Mej. Jen. Richard M. Makanzo (Misri).


Chapisha Maoni

0 Maoni