Rais wa zamani Ghana ashinda urais akiwa upinzani

 

Mgombea wa upinzani na Rais wa zamani wa Ghana John Dramani Mahama ametangazwa rasmi kuwa mshindi katika uchaguzi wa urais Ghana uliofanyika mwishoni mwa juma.

Mahama alijipatia ushindi wa asilimia 56.6 za kura zote zilizopigwa huku mpinzani wake makamu wa Rais wa sasa Mahamudu Bawumia akiambulia asilimia 41.6 ya kura.

Ni ushindi mkubwa zaidi katika nchi hiyo kwa miaka 24. Waliojitokeza kupiga kura walikuwa ni asilimia 60.9, alisema Mkuu wa Tume ya Uchaguzi nchini Ghana, Jean Mensa.

Mahama amesema anahisi “kufurahishwa” na kwamba yeye na chama chake cha National Democratic Congress (NDC). “Wamepiga kura moja ya matokeo mazuri katika historia ya uchaguzi wa Ghana.”

Mahama aliahidi kuleta “mwanzo mpya, mwelekeo mpya” na akabainisha kuwa Ghana imeweka historia kwa kumchagua makamu wa rais wa kwanza mwanamke Jane Naana Opoku Agyemang.

Chapisha Maoni

0 Maoni