Rais Samia afichua siri, Janabi kuwania nafasi ya Ndugulile

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amemtaka Mkurugenzi Mtandaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Prof. Mohamed Janabi kujiandaa kugombea nafasi ya aliyekuwa Mkurugenzi wa Shirika la Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika, Dkt. Faustine Ndugulile.

Dkt. Janabi ambaye ameteuliwa na Rais hivi karibuni kuwa Mshauri wa Rais Masuala ya Afya na Tiba, ameambiwa kujianda kwa nafasi hiyo ya Dkt. Ndugulile ambaye pia alikuwa Mbunge wa Kigamboni, aliyefariki dunia Novemba 27, 2024 ikiwa ni miezi kadhaa kupita tangu ashinde nafasi hiyo.

Akizungumza mara baada ya kuwaapisha viongozi mbalimbali leo Desemba 10, 2024 kwenye Ikulu Ndogo ya Tunguu, Zanzibar, Rais Samia amesema wamepitia wasifu nyingi na kubaini kwamba, Profesa Janabi ana sifa ya kurithi mikoba ya marehemu Dkt. Ndugulile.

“Naomba nifichue siri hapa, tumepitia CV kama tano na tukaona Prof. Janabi anafaa kuchukua nafasi ya Dkt. Ndugulile, Hivyo, tunakundaa kwenda kugombea nafasi hiyo muda utakapofikia. Ujiandae,” amesema Rais Samia.

Chapisha Maoni

0 Maoni