Polisi yafuatilia tukio la kutekwa Nondo wa ACT

 

Jeshi la Polisi limesema kwamba linafuatilia tukio la kutekwa Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Ngome ya Vijana, Abdul Nondo baada ya kupokea taarifa hiyo leo Desemba mosi 2024 na kufungua jalada.

Nondo anadaiwa kutekwa leo alfajiri katika stendi ya Magufuli eneo la Mbezi Louis wakati akiwasili kutokea mkoani Kigoma kwa usafiri wa basi la Saratoga lenye namba za usajili T 221 DKB.

Nondo alikuwa sehemu ya viongozi wa kitaifa wa chama hicho walioongoza kampeni za uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwenye mikoa ya magharibi mwa Tanzania.

Taarifa iliyotolewa leo na Msemaji wa Jeshi la Polisi DCP David Misime imepokea taarifa ya kutekwa kwa mtu mmoja mwanaume katika stendi ya Magufuli Mbezi Louis Dar es Salaam.

Taarifa hiyo imesema mtu huyo ametekwa kwa nguvu majira ya saa 11:00 alfajiri na kuchukuliwa na watu waliokuwa wakitumia gari lenye usajili namba T 249 CMV aina ya Landcruise rangi nyeupe.



Chapisha Maoni

0 Maoni