Kiongozi
Mkuu Mstaafu wa ACT Wazalendo Zitto Kabwe amemtembelea Mwenyekiti wa Ngome ya
Vijana wa chama hicho Abdul Omary Nondo katika hospitali ya Aga Khan na kusema
kuwa hali yake bado si nzuri na anaendelea na matibabu.
Zitto
amesema kwamba kwa sasa Nondo anaendelea na matibabu na hali yake itakapotengemaa
ndipo ataweza kuelezea tukio hilo lililomkuta, “Tunaamini hapa alipo yupo
katika hospitali sahihi kwa matibabu yake atakapopona ataongea.”
Nondo alitekwa
jana leo alfajiri katika stendi ya Magufuli eneo la Mbezi Louis wakati
akiwasili kutokea mkoani Kigoma kwa usafiri wa basi la Saratoga lenye namba za
usajili T 221 DKB.
Kufuati
tukio hilo Jeshi la Polisi limesema kwamba linafuatilia tukio la kutekwa Nondo
baada ya kufungua jalada, hata hivyo jana usiku Nondo alipatikana akiwa
ametelekezwa kwenye fukwe ya Coco huku akiwa na maumivu makali.
Taarifa ya
Polisi iliyotolewa leo Desemba 2, 2024 na msemaji wake, David Misime imesema baada ya kutelekezwa katika fukwe hizo,
aliomba msaada wa bodaboda kumfikisha katika ofisi za chama chake Magomeni, Dar
es Salaam.
"Desemba
mosi, 2024 majira kama saa nne na nusu usiku Abdul Omary Nondo ambaye tulikuwa
tunamtafuta kwa kushirikiana na watu mbalimbali, wakiwepo viongozi wake wa
chama cha ACT Wazalendo baada ya kukamatwa na kuchukuliwa kwa nguvu pale kituo
cha mabasi cha Magufuli, ameeleza alitelekezwa maeneo ya fukwe za Coco (Coco
Beach) Kinondoni, Jijini Dar es Salaam na watu asiowafahamu.
"Baada
ya kutelekezwa alisimamisha bodaboda na kumwelekeza amfikishe katika ofisi za
chama chake zilizopo Magomeni, Jijini Dar es Salaam na walifika muda wa saa
tano usiku,” imeeleza tarifa hiyo na kuongeza kuwa alionana na viongozi wake na
kupelekwa hospitali kwa ajili ya uchunguzi wa afya yake.

0 Maoni