Nondo asimulia mazito aliyofanyiwa na watekaji

 

Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana wa chama cha ACT Wazalendo Abdul Nondo amevunja ukimya na kuongelea kwa mara ya kwanza tukio la kutekwa na watu wasiokulikana katika stendi ya mabasi ya mikoani na nchi za nje ya Magufuli Mbezi Loius Jijini Dare s Salaam.

Nondo alitekwa Novemba 30, 2024 alfajiri katika stendi hiyo wakati akiwasili kutokea mkoani Kigoma kwa usafiri wa basi la Saratoga lenye namba za usajili T 221 DKB na kuchukuliwa na gari lenye usajili namba T 249 CMV aina ya Landcruise rangi nyeupe.

Akiongea kwa uchungu akiwa hospitali ya Aga Khan ambayo amelazwa akipatiwa matibabu, Nondo amesema alijikuta akizingira na watu wapatao sita alipotoka tu nje ya kituo hicho na wakamuambia yupo chini ya ulinzi, akae kimya asipige kelele.

“Watu hao walinizingira na mwanzo nilidhani kuwa ni vibaka walipoanza kunikamata kwa nguvu nilipiga kelele kuomba msaada kwa watu lakini hakuna aliyekuja kunisaidia mara nikaona gari nyeupe ikija na kunipakia,” alisema Nondo.

Amesema akiwa kwenye gari watu hao waliulizana kuwa pingu zipo wapi na walipozikosa walimfunga kwa kamba mikono yake kwa nyumba na kisha kumfunga kitambaa machoni asione na kuondoka naye.

Amesema lifikapahali akashushwa kwenye jengo na kisha kuanza kupigwa na marungu kwenye magoti, kwenye nyao na kwenye mabega, huku wakimuambi kuwa yeye anajifanya kuwa chamdomo hivyo leo watamuua.

“Baada ya kipigo hicho zililetwa pingu nikafungwa na kisha miguu yangu ikaingizwa bomba kati kati nikaning’inizwa kichwa chini miguu juu na kuendelea kuteswa kwa kupatiwa kipigo,” alisema Nondo.

“Nikiwa katika eneo hilo nilikuwa nasikia watu kama wakizungumza milio ya magari ikipita pamoja na ving’ora vya Ambulance (gari la wagonjwa) hali iliyonifanya kujua kuwa nilipo sipo mbali na barabara,” alisema Nondo.

Amesema kwamba watekaji hao walibadilisha gari na kumchukua hadi eneo la fukwe ya Coco, ambayo alikuja kulitambua baadae baada ya kufunguliwa kitambaa na mikondo iliyofungwa na kutelekezwa.

Amesema kwamba watekaji hao walimueleza aende nyumbani moja kwa moja na asiongee na vyombo vya habari la sivyo watakuja kumteka mahala popote atakapokuwapo na safari hii hawatomuachia hai watamuua.

Chapisha Maoni

0 Maoni