Nabii Elvis Mbonye wa Uganda amtabiria mema Rais Ramia

 

Nabii maarufu nchini Uganda na Duniani Prophet Elvis Mbonye, ametabiria mambo mema Rais SSH, kwamba utawala na mamlaka yake yatazidi kushamiri na kupanuka mpaka nje ya Tanzania.

Amesema hayo leo Jijini Dar es Salaam, katika mkutano wake na viongozi mbalimbali wa makanisa pamoja na serikali uliofanyika ukumbi The Dome, Masaki.

Amesema aliamua kuja Tanzania, ili kukutana makuhani wa Mungu, ili awape ujumbe ambao Bwana Mungu amempa mahsusi kwa ajili ya nchi ya Tanzania.

 "Bwana Mungu amenimbia kwamba nchi ya Tanzania inaenda kungara sana,na itang'ara chini ya Uongozi wa Rais huyu mliyenaye.Siyo hivyo tu, lakini pia uongozi wa Rais huyu utaenda kukua na kushamiri mpaka nje ya hapa kwenu.Yatunzeni vizuri haya  maneno niyasemayo leo hii."

Miongoni mwa viongozi wa serikali waliohudhuria mkutano huo ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila.

Katika salamu zake kwa niaba ya serikali, Bw Chalamila amesema uhusiano wa Uganda na Tanzania una historia ndefu na hakuna mtu yeyote atayeweza kuuharibu.

"Nakumbuka nilipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera tulikuwa tuna mikutano ya mara kwa mara ya ujirani mwema, tukijadili mambo nuhimu ya kuziendeleza nchi zetu hasa kule pembezoni mipakani.Uhusiano huo utazidi kuendelea maana sisi ni ndugu," amesema.

Kwa mujibu ya video zake ilizoko Youtube, Nabii huyu amewahi kutabiri mambo mbalimbali, likiwemo la kuondolewa wa Waziri Mkuu wa Uingereza Rish Sunak, ambapo alitoa utabiri huo miezi mitano kabla Waziri Mkuu huyo hajajiondoa madarakani.

Aidha, alitabiri kurejea tena madarakani kwa Rais Donald Trump wa Marekani, jambo ambalo alilifanya mwaka mmoja na nusu kabla ya uchaguzi wa Marekani uliofanyika mwaka huu.

Aliwahi pia kutabiri kutokea kwa mafuriko ya nchini Dubai, jambo ambalo alilifanya miezi mingi kabla tukio hilo halijatokea.Jambo hilo kweli lilikuja kutokea mwaka huu.

Nabii Mbonye alitabiri pia mafuriko ya kaskazini mwa Kenya miezi mitano kabla hayajatokea.Na lilipokuja kutokea lilisababisha maafa makubwa nchini humo.

Aidha, Nabii huyo pia aliwahi kutabiri kwamba ndege mbili za Uganda zingeanguka nchini Somalia.Baada ya utabiri huo aliijulisha Serikali ili wasipeleke ndege huko Somalia.Hata hivyo serikali ya Uganda walimpuuza, na kweli ndege hizo zilipokwenda huko ilikuja kutokea kweli kama alivyotabiri maana ziliangushwa.

Nabii Mbonye ana mvuto mkubwa kwa watu wa rika zote nchini Uganda,lakini zaidi zaidi vijana ambao wanakwenda kwake ili kutatuliwa matatizo yao ya kiroho na kimwili.

Mkutano wake wa Dar es Salaam uliandaliwa na Umoja wa Makanisa ya Mitume na Manabii Tanzania, chini ya uongozi wa Rais wa Makanisa hayo Nabii Joshua.

Gharama zote za maandalizi za mkutano huo zikiwemo za ukumbi, kifungua kinywa na nyinginezo zimegharimiwa na Nabii huyo wa Uganda ambaye pia ana ukwasi mwingi.

Chapisha Maoni

0 Maoni