Mwekezaji kiwanda cha KEDA ajenga daraja la Mto Msorwa

 

Mwekezaji kiwanda cha KEDA Tanzania Ceramic Company Limited kimetekeleza ujenzi wa mradi wa ujenzi wa daraja katika Mto Msorwa uliopo barabara ya Mbezi Msorwa Shungubweni Boza yenye urefu wa mita 6 upana mita 7 kina mita 1.5 eneo la Mto Msorwa barabara inayoungansiha kata ya Mbezi na Shungubweni mradi unaotokana na fedha za kurudisha fadhila kwa jamii katika kuunga mkono jitihada za Rais Samia katika kusaidia wananchi kwenye maeneo yenye uwekezaji ili nao wanufaike.

Akizungumza katika eneo la mradi huo Afisa Biashara Kiwanda cha KEDA Bw. Masoud Suleyman amesema mradi huo wa kuimarisha miundombinu ya barabara utawezesha kata ya Mbezi Shungubweni kurahisisha shughuli za kiuchumi na huduma za kijamii kwa wananchi wa kata hizo na kurahisisha usafirishaji wa malighafi ya mchanga katika utengenezaji wa bidhaa ya kioo.

"Gharama za mradi umetekelezwa kwenye kutumia fedha za ufadhili wa kiwanda cha KEDA Ceramics Tanzania Companya Limited kwa mwaka 2024 gharama ya mradi ikiwa  ni shilingi milioni 150  ambapo utekelezaji wake mradi huo umejengwa kwa kutumia wataalamu,vifaa na malighafi za kiwanda cha KEDA,"  amesema Sulyman na kuongeza kuwa,

"Utekelezaji wake umeanza tangu tarehe 28/10/2024 kwa kushirikiana na wataaalamu kutoka ofisi ya Meneja Tarura Wilaya ya Mkuranga vifaa na malighafi za kiwanda vimetolewa na kiwanda cha KEDA, manufaa ya mradi utawezesha wananchi kupita kiurahisi kipindo chote cha mwaka kama misimu ilivyo ikiwemo kipindi cha mvua."

Kwa upande wao baadhi ya wananchi katika vijiji tofauti vilivyonufaika na mradi huo akiwamo Mohammed Msumi mkazi wa kitongoji cha kikopi kijiji cha Msolwa anasema walikuwa wakipata tabu kuvuka katika eneo hilo haswa katika kipindi cha mvua.

"Vijana walikuwa wakivusha watu kwa pesa lakini KEDA wameona tatizo wamelipanua daraja hili katika ubora mzuri tunawakaribisha wawekezaji wengine watusaidie ujenzi wa barababara na daraja tunawashukuru sana wawekezaji kwa ukarimu wao," alisema.

Naye Amina Mohammed Juma waliwashukuru wawekezaji wa KEDA kwa kuwajengea daraja ambalo lilikuwa  korofi wakati wa mvua eneo hujaa maji na wananchi magari kukwama kwa kushindwa kupita hali iliwanyima usingizi wananchi wanaotumia barabara hiyo kwa muda mrefu na kuchangia maendeleo yao kurudi nyumba.

Nao baadhi ya viongozi wateule wa serikali za vijiji kikiwemo Msolwa lilipo daraja hilo,  Jumanne Mtambwe ni Mwenyekiti Mteule kijiji cha Kisayani Mkuranga  amesema wanafurahia ujenzi huo kwa kuwa umewanunganisha kijiji cha Kisayani Msolwa na Shungubweni amesema ujenzi huo utaleta chachu ya maendeleo kwa kuwa barabara sasa zitapitika vizuri kwani tatizo la daraja limetatuliwa.

 "Tunawashukuru KEDA lakini pia tunawaomba watujengee barabara ambayo kwa sasa inasumbua kutokana na kasi ya magari yanayobeba mchanga ambao ni malighafi ya bidhaa ya vioo ambayo inatumika katika kiwanda chao, tunamuombea pia Rais Samia aendelee kuvutia uwekezaji nchini kwetu ili fursa zifunguke na wananchi tuwe na maendeleo endelevu kama walivyofanya KEDA," alisema mtambwe.




Chapisha Maoni

0 Maoni