Mwanamke achomwa moto na kufa kwenye treni New York

 

Mwanaume mmoja amekamatwa Jijini New York nchini Marekani kwa kuhusika na kifo cha mwanamke aliyechomwa moto kwenye treni ya aridhini.

Kamishna wa Polisi Jessica Tisch ameelezea tukio hilo la Jumapili kama moja ya matukio ya kihalifu ambayo mtu huwezi kuamini anaweza kumtendea binadamu mwenzake.

Kamishna Tisch ameeleza kuwa mwanamke huyo akiwa kwenye treni iliyosimama huko Brooklyn alifuatwa na mwanaume huyo aliyetumia kibiriti kuwasha moto nguo zake.

Amesema mwanamke huyo alikufa papo hapo kwenye treni, na kuongeza kuwa mhusika amekamatwa. Hakukua na maongezi yoyote baina yao kabla ya kuchomwa moto.



Chapisha Maoni

0 Maoni