Mambo yalivyobamba Ruhila Zoo siku ya Boxing Day

 

Wakazi wa Manispaa ya Songea wamejitokeza kwa wingi kuvinjari ndani ya Bustani ya Wanyamapori hai RUHILA katika siku ya kufungua zawadi za Sikukuu ya Krismasi maarufu kwa lugha ya Kingereza kama "Boxing Day".

Jumla ya watalii wa ndani 178 waliweza kutembelea bustani hiyo na kupata fursa ya kujionea wanyamapori mbalimbali waliopo ndani ya bustani hiyo ikiwa ni pamoja na kufurahia muziki wa kumtoa nyoka pangoni wa Live Band mashuhuri kutoka Manispaa hiyo.

Mbali na burudani hizo watalii,  kulikuwa na nafasi mahsusi kwa watoto kucheza michezo mbalimbali kwa kutumia vifaa vya kisasa zikiwemo "Jumping Castle", magari ya watoto, swimming pool na mambo kadha wa kadha ya kuondoa msongo wa mawazo  kubwa zaidi ni kujipatia Nyamapori Choma iliyoandaliwa kwa viwango vya kufunga mwaka.

Watu waote mnakaribishwa RUHILA ZOO iliyopo katikati ya Manispaa ya Songea... “kwetu sisi furaha yako ndiyo kipaumbele chetu.”

Wasiliana naoa kwa namba +255 676 475 541 (Afisa Habari wa TAWA) au +255 767 228 414 (Afisa Utalii wa Ruhila ZOO).



Chapisha Maoni

0 Maoni