Dkt. Biteko ahimiza elimu ya matumizi ya nishati kwa ufanisi

 

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko amesema upotevu wa nishati bado ni mkubwa, hivyo mikakati ya kukabiliana na upotevu huo ni muhimu ili kujenga jamii inayotumia nishati kwa ufanisi zaidi.

“Tunahitaji kukabiliana na suala hili kwa kuzingatia mikakati ya matumizi bora ya nishati ambayo tutaidhinisha hapa leo, Ninawahakikishia wadau wote kwamba Wizara ya Nishati na Serikali ya Tanzania ziko tayari kusaidia kufanikisha malengo haya ya kimkakati,” amesma Dkt. Biteko.

Dkt. Biteko amayasema hayo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Kikanda wa Matumizi Bora ya Nishati unaoendelea PAPU Tower Disemba 4, 2024 Jijini Arusha.



Chapisha Maoni

0 Maoni