Bodi ya NHC yapongeza miradi ya nyumba za makazi kongwa


Bodi ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) imekagua miradi ya serikali katika Wilaya ya Kongwa na kutembelea nyumba zilizofanyiwa ukarabati mkubwa. Nyumba hizi za gharama nafuu zimepangishwa kwa wananchi na sasa zinauzwa kupitia utaratibu wa Mpangaji Mnunuzi.

Mradi huu ni sehemu ya juhudi za NHC kuhakikisha wakazi wa Kongwa wanapata makazi bora, salama, na yenye gharama nafuu. 

Hii ni hatua kubwa katika kuboresha maisha ya Watanzania na kuchochea maendeleo katika wilaya hii. Ziara hiyo imefanyika baada ya kukamilisha ukaguzi wa miradi ya serikali inayotekelezwa na NHC katika mji wa serikali Mtumba.

Kuwa sehemu ya mafanikio haya, Furahia fursa ya kumiliki nyumba yako kupitia mpango huu wa kipekee wa Mpangaji Mnunuzi. Tembelea NHC leo na jifunze zaidi.

Chapisha Maoni

0 Maoni