Basi lililobeba wabunge lapata ajali Dodoma

 

Basi lililokuwa limewabeba wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania waliokuwa wakielekea Kenya limegongana na lori la mizigo maeneo ya Mbande, Kongwa mkoani Dodoma asubuhi ya leo Desemba 06, 2024.

Wabunge hao walikuwa wakielekea Kenya kushiriki mashindano ya michezo ya Mabunge ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Majeruhi wa ajali hiyo wamekimbizwa katika Hospitali ya Uhuru na Hospitali ya Benjamin Mkapa zote za mkoani Dodoma. Tuataendelea kuwaletea taarifa zaidi.

Chapisha Maoni

0 Maoni