Shirika
kongwe la Uhifadhi nchini (TANAPA) na Bodi ya Utalii (TTB) ni miongoni wa
taasisi kutoka nchini Tanzania wanaoshiriki Maonesho ya Kimataifa ya Utalii na
Utamaduni ya GITA MAHOTSAV yanayoendelea katika Mji wa Kurukshetra Jimbo la
Haryana nchini India.
Maonesho
hayo yalitanguliwa na maonesho ya kiimani/kidini kwa wananchi wa mji Mtakatifu
wa Kurushektra yaliyoanza tarehe 28 Novemba, 2024 mpaka 4 Desemba, 2024 ambayo
yalitoa nafasi kwa washiriki kutoka Tanzania kujifunza Imani ya watu wa India
ambao wana Miungu takribani Milioni thelathini.
Ushiriki wa
Tanzania ni kufuatia mwaliko wa Jamhuri ya watu wa India ambayo imekuwa na
urafiki na uhusiano mzuri wa kindugu na kidiplomasia kwa muda wa zaidi ya miaka
60.
Hafla ya
ufunguzi imehudhuriwa na Mheshimiwa Tabia Maulid Mwitta - Waziri wa Utalii
Michezo na Utamaduni kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Mhe. Waziri
akiwa na mwenyeji wake (Mkuu wa Jimbo la Haryana) na viongozi wa nafasi za juu
kutoka Serikali ya India na Jimbo la Haryana walipata nafasi ya kutembelea
Banda la Tanzania ambapo maelezo kuhusu vivutio, fursa za uwekezaji na Utalii
yalitolewa vikiambatana na zawadi maalum kwa wageni kama sehemu ya ukarimu
ambao nchi imejaaliwa.
Nchi ya
India ni miongoni mwa masoko ya kimkakati kiutalii ambapo ushiriki wa Tanzania
utasaidia kufikia idadi ya watalii milioni tano ifikapo 2025/2026.
Aidha uwepo
wa fursa za uwekezaji utatoa nafasi kwa watu wenye sifa na mitaji kuwekeza
katika maeneo ya malazi na mazao ya Utalii kama wanavyoendelea kutangaza washiriki hao.
Kwa upande
wa Tanzania Maonesho hayo yanawakilishwa na Shirika la Hifadhi za Taifa
Tanzania (TANAPA), TTB na maofisa kutoka ubalozi wa Tanzania nchini India.
Maonesho
hayo yanayotarajiwa kufungwa rasmi kimataifa tarehe 11.12.2024 lakini kwa
washiriki kutoka mataifa mbalimbali kuendelea na Maonesho ya kunadi bidhaa zao
hadi Desemba 15, 2024 ili kutoka fursa zaidi kwa nchi washiriki kuendelea
kupata masoko na kubasilishana uzoefu wa kibiashara.
0 Maoni