Assad yasemekana yupo Urusi na familia yake

 

Rais wa Syria Bashar al-Assad na familia yake wamewasili Jijini Moscow, vyombo vya habari vya serikali ya Urusi vimeripoti, vikinukuu vyanzo vya habari katika Ikulu ya Kremlin.

Assad ambaye ameondolewa madarakani, aliondoka jana Damascus kwa ndege bila kujulikana anaelekea wapi. Inadaiwa yeye na familia yake wamepewa hifadhi Urusi.

Hata hivyo taarifa hizo kutoka Urusi, hazijathibitishwa na vyombo mbalimbali vya habari vya kimataifa, ingawa inajulikana kuwa Assad amekuwa mshirika wa karibu na Urusi.

Na ni silaha kali za Urusi zilizomsaidia kumuweka Bashar al-Assad madarakani kwa miaka tisa iliyopita.

Wakati huo huo, Urusi imeomba mkutano wa dharura wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ili kujadili hali nchini Syria, kwa mujibu wa mmoja wa wawakilishi wake.

Chapisha Maoni

0 Maoni