Waziri Mkuu azindua kamati ya uchunguzi wa jengo la Kariakoo

 

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa amezindua kamati ya wataalamu ya uchunguzi wa jengo lililoporomoka katika eneo la Kariakoo ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuchunguza chanzo cha tukio hilo pamoja na kufahamu ubora na uimara wa majengo yote yaliyoko Kariakoo.

Waziri Mkuu Majaliwa amekutana na wajumbe wa kamati hiyo leo jijini Dar es Salaam na kuwataka wahakikishe wanafanya uchunguzi wa kina, uwazi, haki na kwa kuzingatia viwango vya kitaaluma.

“Fanyeni kazi hii kwa weledi, Taifa limewatuma nendeni mkaifanye kazi hii na mlete matokeo,” amesema Majaliwa huku akiiagiza itekeleze majukumu yake kwa kufuata sheria, kanuni na maadili ya kazi.

Jumamosi ya Novemba 16, 2024, jengo hilo lililopo Kariakoo jijini Dar es Salaam liliporomoka na kusababisha vifo vya watu 20 hadi sasa pamoja na majeruhi zaidi ya 86.






Chapisha Maoni

0 Maoni