Waziri Mkuu aagiza kutumika oksijeni uokoaji Kariakoo

 

Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa amesema katika kufanya jitihada za uokoaji, ameagiza mitungi ya gesi ya oksijeni kutumika kwa ajili ya kupeleja hewa safi kwa waliokwama kwenye vifusi.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo Novemba 16, wakati alipofika Mtaa wa Kongo, Kariakoo kufuatia tukio la jengo la ghorofa kuporomoka na kufukia baadhi ya wafanyabiashara na wateja.

"Uzuri tunaambiwa kuwa baadhi ya familia zinapata mawasiliano na ndugu walioko huko chini (kwenye vifusi). Kwa hiyo jitihada zinaendelea za kuwaokoa waliopo huko chini, tuhakikishe hatutumii nguvu bali tunatumia akili zaidi ili tuweze kuokoa maisha yao.”

"Kwa sasa wanakosa hewa lakini tumeandaa utaratibu wa kupeleka oksijeni kiasi cha kutosha ili waliopo kule waweze kudumu kwa muda mrefu, wakati tukiendelea na zoezi la uokoaji," amesema Mhe. Majaliwa.

Ameeleza kwamba katika zoezi hilo la uokoaji hadi anapoongea jumla ya watu 28 walikuwa wameshaokolewa wakiwa hai na kupelekwa hospitali kupatiwa matibabu, huku mtu mmoja akithibitishwa kufa.

Chapisha Maoni

0 Maoni