Muhimbili yapokea majeruhi 40 ajali ya ghorofa Kariakoo

 

Hospitali Kuu ya Taifa ya Muhimbili imethibitisha kupokea majeruhi 40 wa ajali ya kuporomoka kwa ghorofa iliyotokea mapema leo Kariakoo Mtaa wa Kongo jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa hospitali hiyo Prof. Mohamed Janabi amesema tayari majeruhi 32 kati ya hao wamepatiwa matibabu na kuruhusiwa kurejea nyumbani huku wengine wanane wakiendelea kupatiwa matibabu.

Pamoja na Muhimbili, hospitali nyingine za umma zinazozendelea kupokea majeruhi wa ajali hiyo na kuwahudumia ni hospitali ya rufaa ya wilaya ya Ilala, Amana pamoja na hospitali ya Mnazi Mmoja.

Chapisha Maoni

0 Maoni