Ghorofa laporomoka na kufukia watu kadhaa Kariakoo

 

Watu kadhaa wanahofiwa kuwa wamefukiwa na kifusi baada ya jengo moja la ghorofa lililopo Kariakoo Mtaa wa Kongo na Mchikichi jijini Dar es Salaam kuporomoka.

Mashuhuda wameeleza kuwa jengo hilo la biashara lileporomoka leo Jumamosi, ambapo inahofiwa kuwa kuna watu walikuwamo katika eneo la chini wakati likiporomoka.

Wameeleza kuwa kunawafanyabiashara na watu kadhaa walikokuwa wanafanya manunuzi katika maduka ya jengo lililoporomoka.

Polisi kwa kushirikiana na wananchi wanaendelea na jitihada za uokoaji, ili kunusuru maisha ya watu waliofukiwa na kifusi.

Chapisha Maoni

0 Maoni