Rais mteule Trump amteua Mtendaji Mkuu wa Ikulu

 

Rais mteule wa Marekani Donald Trump amemteua meneja wake wa kampeni Susan Summerall Wiles kuwa Mtendaji Mkuu katika Ikulu ya Marekani (White House).

Trump amesema katika taarifa yake kwamba Wiles "alinisaidia kufikia ushindi mkubwa zaidi wa kisiasa katika historia ya Marekani.”

Kulingana na kambi ya Trump, Wiles atakuwa mwanamke wa kwanza kuhudumu katika nafasi hiyo.

Susie Wiles, anaelezewa kama mshirika wa kisiasa anayeogopwa zaidi na anayejulikana sana Marekani na vyombo vya habari nchini humo.

Chapisha Maoni

0 Maoni