Prof. Muhongo atoa nondo za kukuza uchumi bungeni

 

Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini, Prof Sospeter Muhongo ameongelea vipaumbele muhimu vya kukuza uchumi wa Taifa kwa kiwango cha asilimia kumi (10%)

Akichangia hoja Bungeni leo jijini Dodoma Prof. Muhonga amesema, “Huko vijijini kwa wakati huu hii bajeti tunayoitaarisha mwakani maeneo matatu lazima tuyawekee mkazo sana; nayo ni maji, umeme na barabara.”

“Nadhani bajeti tutakayoitayarisha mwakani itazingatia hayo, lakini tunamiradi mingi huenda fedha zisitoshe, napendekeza mbali ya fedha za makusanyo ya TRA tuanze mazungumzo na mabeki ili tuweze kukopa kwa riba ndogo na pengine tupate fedha kwenye Stock Exchange (Soko la Hisa).”

Aidha, Prof. Muhongo, amelieleza bunge kuwa kuna fursa nyingi za ajira nchi za nje ambazo zinahitaji wageni mabingwa wenye utaalam, na kuongeza kuwa wasiowataka kule ni hawa wakimbizi.

Amesisitiza kuwekeza zaidi katika masomo ya Sayansi ili kuzalisha wataalamu wabobezi ambao sio tu watakazana kutafuta ajira za ndani pekee, bali pia wataweza kuingia katika soko la ajira za nje.

Ili tutoke kwenye ukuaji wa uchumi wa asilimia 5-6 kwenda kwenye uchumi wa asilimia 10, mimi nafikiri ni lazima sasa tuwekeze kwenye maeneo manne, kwanza elimu iandane na ajira, tuwekeze kwenye uchumi wa hellium na gesi, kwenye kilimo cha biashara madini na utalii, ameshauri Prof. Muhongo.

Pamoja na mambo mengine Prof. Sospeter Muhongo, ameishukuru Serikali kwa utekelezaji wa miradi miwili mikubwa jimboni mwake.

“Mheshimiwa Rais alipokuwa jimbo la Musoma Vijijini nilimuomba miradi mikubwa miwili barabara ya Km 92 na kufufua kilimo kikubwa cha umwagiliaji nashukuru kwamba vyote vimefanikiwa pongeze kwake na pongezi kwa TANROADS,” alisema Prof. Mugongo.

Ameeleza kuwa barabara hiyo kwa wakati huo ilikuwa na gharama ya dola milioni 150 matangazo yametoka wakandrasi wengi wameshabikia na sasa wapo katika hatua ya manunuzi.

Prof. Muhongo ameongeza kuwa barabara hiyo ina daraja ambalo ujenzi wake utagharamiwa na World Bank (Benki ya Dunia) ambapo lipo katika hatua ya manunuzi, nalo pia litakamilishwa.

Kuhusu Kilimo cha Umwagiliaji nashukuru Mhe. Hussein Bashe na Wizara ya Kilimo wanaenda vizuri hivi karibuni nadhani mwakani tunaanza kujenga miundombinu ya umwagiliaji,” amesema Prof. Muhongo.

Chapisha Maoni

0 Maoni