Rais Mstaafu Kikwete apiga kura Kijijini Msoga

 

Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Jakaya Mrisho Kikwete leo ameshiriki zoezi la kupiga kura katika uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji katika kijiji cha Msoga Halmashauri ya Chalinze wilayani Bagamoyo Pwani ikiwa ni haki ya msingi ya kumpata kiongozi aneedhani kuwa ataleta maendeleo katika kijiji chake.

Mh. Kikwete aliwasili majira ya saa nne asubuhi katika kituo cha Kota kilichopo kijiji cha msoga na kupiga kura ikiwa ni sehemu ya kutekeleza demokrasia inayolenga kumpata mwenyekiti na wajumbe huku akieleza kufurahishwa na idadi ya wananchi waliojitokeza kupiga kura kwani hii inaonesha namna wananchi walivyohamasika kushiriki katika uchaguzi.

Mbunge wa jimbo la Chalinze Ridhiwan Kikwete kufurahishwa na utaratibu mzuri uliowekwa na serikali ya kuhakikisha wananchi wanapiga kura kwa amani na utulivu.

Mmoja wa wagombea katika uchaguzi huo Hasasan Shaban akaeleza kuwa kutokana na kijiji hicho kutokua na wagombea kwa upande upindi matumaini yake kuwa ataibuka na ushindi kwa kupata kura nyingi za ndio ili awatumie wananchi wa eneo hilo.

Chapisha Maoni

0 Maoni