Rais Kiir awasili Arusha kushiriki mkutano wa EAC

 

Rais wa Jamhuri ya Sudan Kusini na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), Mhe. Salva Kiir Mayardit, amewasili nchini Tanzania leo kwa ajili ya kushiriki katika Mkutano wa 24 wa Wakuu wa Nchi wa EAC.

Mkutano huu unafanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC), Arusha, leo tarehe 30 Novemba 2024.

Mhe. Rais Kiir alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), alipokelewa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Selemani Jafo.

Chapisha Maoni

0 Maoni