Polisi Songwe wamkabidhi mdude kwa Polisi Mbeya

 

Jeshi la Polisi Mkoani Songwe limesema limekamilisha mahojiano na kada wa CHADEMA, Mdude Nyangali na wamempeleka mkoani Mbeya kwa mahojiano mengine na jeshi hilo kujibu tuhuma zinazomkabili.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Kamanda wa Polisi mkoani Songwe, Agustino Senga, amesema tayari wamemaliza mahojiano na mwanaharakati huyo, na tayari ameelekea Mbeya kujibu tuhuma nyingine zinazomkabili.

Nyagali alikamatwa Novemba 22, 2024 mkoani Songwe akiwa na makada wengine wa Chadema akiwamo Mwenyekiti wake Taifa, Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Kanda ya Nyansa, Joseph Mbilinyi 'Sugu' kwa madai ya kukiuka taratibu za kampeni za uchaguzi wa Serikali za Miraa.

Hata hivyo, makada wengine waliachiwa na Polisi wakiwamo Mwenyekiti wake Taifa, Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Kanda ya Nyansa, Joseph Mbilinyi 'Sugu', ila Mdude aliendelea kushikiliwa kwa ajili ya mahojiano.

Chapisha Maoni

0 Maoni