Pelosi amtupia lawama Biden kushindwa kwa Democrats

 

Aliyekuwa Spika wa Bunge la Wawakilishi la Marekani Bi. Nancy Pelosi amesema Chama cha Democrats kingeweza kufanya vizuri katika uchaguzi wa rais iwapo Rais Joe Biden angejitoa mapema kwenye kinyang’anyiro.

Pelosi mmoja wa wanasiasa wenye nguvu Washington, ameliambia jarida ya New York Times kwamba “Iwapo rais angejitoa mapema, kungeweza kuwapo na wagombea wengine kwenye mbio za urais.”

Kauli yake hiyo imekuwa ya kwanza ya kushutumiana ndani ya chama cha Democrats baada ya chama hicho kushindwa kuendelea kuwapo Ikulu na kunauwezekano wa kupoteza nafasi za kwenge Baraza la Congress Jumanne.

Chapisha Maoni

0 Maoni