Mkurugenzi Mtendaji wa Dar24 Media apatikana

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Dar24 Media na Mfanyakazi wa Kampuni DataVision International Limited, Maclean Godfrey Mwaijonga, aliyeripotiwa kupotea Oktoba 31, 2024 baada ya kutoka ofisini kwake amepatikana.

Akiongea na waandishi wa habari, Kamanda wa Jeshi la Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Muliro Jumanne amesema Mwaijonga amepatikana jana Kigamboni akiwa katika hali ya kutokua na nguvu ambayo inatokana na kunywa kinywaji kinachosadikika kuwa na kitu kilichopoteza fahamu zake.

 “Jioni ya leo (jana) tumepokea taarifa kutoka kwa ndugu wa karibu kuwa Mwaijonga ameonekana Kigamboni, tukaongozana na familia mpaka huko Buyuni na kumkuta akiwa hana nguvu, tukampeleka Hospitali tunashukuru hana tatizo,” amesema Kamanda Muliro.

Mwaijonga inadaiwa alipotea Oktoba 31, 2024 wakati anatoka ofisini kwake eneo la Rose Garden, Mikocheni jijini Dar es Salaam akiwa na gari yake aina ya Toyota Prado nyeusi yenye usajili namba T 645 DEE.

Chapisha Maoni

0 Maoni