Mbowe na wenzake waachiwa huru, Mdude bado

 

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema viongozi wake wakuu akiwemo Mwenyekiti wao Freeman Mbowe, ambao walikuwa wanashikiliwa na polisi mkoni Songwe wameachiwa huru bila masharti jana usiku.

Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa CHADEMA John Mrema amesema hata hivyo mwanachama wao Mdude hajaachiwa, “RPC kasema wana mahojiano naye pamoja na mtu mmoja ambaye aliumizwa vibaya na polisi, tunaendelea kufuatilia hali ya afya yake.”

Jeshi la Polisi Mkoani Songwe jana November 22,2024 lilitoa taarifa kuwa linawashikilia Wanachama wa CHADEMA ambao ni Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa Freeman Mbowe, Joseph Mbilinyi (Sugu) Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Nyasa, Pascal Yohana Haonga, Mbunge Mstaafu CHADEMA Mbozi Mlowo, Mdude Mpaluka Nyagali, Apolinary Boniface Margwe, Afisa Habari CHADEMA na Adam Hassan Kasekwa, Mlinzi wa Mwenyekiti wa CHADEMA.

Wengine waliokamatwa ni Paul Joseph Paul, Afisa wa CHADEMA Kanda ya Nyasa, Mbeya, Kelvin Keneth Ndabila, Afisa habari Kanda ya Nyasa, Mkazi wa Mbeya, Michael Laison Msongole, Mwenyekiti CHADEMA Wilaya ya Mbozi, Mlowo, Mohamed Abdilah Ling wanya, Mlinzi wa Mbowe Mkazi wa Dar es salaam, Alfan Hassan Mbire, Mlinzi wa Mbowe na Ezekia Elia Zambi, Mwenyekiti ACT Wazalendo Mkoa wa Songwe.

Viongozi hao walikamatwa eneo la stendi ya zamani ya Mlowo Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Songwe Novemba 22, 2024 majira ya 10:30 asubuhi baada ya CHADEMA kwenda kufanya mkutano wa kampeni eneo ambalo hawakupangiwa.

Polisi wameeleza kuwa askari waliwapa amri ya kutawanyika lakini walikaidi ndipo polisi walipowatawanya kwa nguvu nao wakaanza kwaurushia mawe polisi na kuwajeruhi askari wawili maeneo ya kichwani, usoni na puani na kwa sasa wanaendela na matibabu Hospitali ya Wilaya ya Mbozi.

Chapisha Maoni

0 Maoni