Dk. Ndugulile afariki dunia nchini India

 

Mbunge wa Kigamboni kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Dk. Faustine Ndugulile amefariki dunia leo Novemba 27, 2024 nchini India alipokuwa akipatiwa matibabu.

Taarifa ya kifo chake iliyotolewa na Spika wa Bunge la Tanzania, Dk Tulia Ackson, imesema taarifa zaidi kuhusu msiba huo zitatolewa baadae.

Dk. Ndugulile alikuwa Mkurugenzi mteule wa Shirika la Afya Dunia Kanda ya Afrika (WHO) ambaye alitarajiwa kuanza rasmi majukumu yake hayo mapya Februari mwakani.

Chapisha Maoni

0 Maoni