Tume ya
Sayansi na Teknolojia Tanzania (COSTECH), imetoa wito kwa wabunifu nchini kupeleka
kazi zao za kibunifu kwenye teknolojia ili waweze kunufaika.
Akizungumza
kwenye kikao na Wahariri leo, Meneja wa NFAST Dk. Beatrice Lymo, amesema, moja
ya kazi ya tume hiyo ni kushindanisha kazi za wabunifu katika teknolojia lakini
pia kutoa mikopo.
“Kati ya
kazi za tume ni kushindanisha wabunifu katika teknolojia, sayansi na tafiti.
Natoa wito kwa wabunifu kuleta kazi na maandiko yao COSTECH ili waweze
kunufaika na mikopo pamoja na mitaji,” amesema.
Dk. Lyimo amesema,
tume hiyo itaingia makubaliano na benki kwa ajili ya kuanzisha Mfuko wa Mikopo
ili kusaidia upatikanaji wa mikopo kwa wabunifu na wavumbuzi.
0 Maoni