Mwenyekiti
wa Chama cha Siasa cha CHADEMA Freeman Mbowe amewataka viongozi wa chama hicho
watakaochaguliwa katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa watende haki kwa wananchi
pindi waingiapo madarakani.
Akiwapigia
kampeni viongozi wa Chadema Mkoani Mbeya, Mbowe amesema kuwa uchaguzi huu
unatoa fursa ya kuwaondoa madarakani viongozi wasiofaa na kuwaingiza madarakani
viongozi wanaofaa kuwatumikia wananchi kwa uadilifu.
"Sisi
CHADEMA tunawachagua viongozi wanaotenda haki, na kama endapo kiongozi wa
CHADEMA aliyechaguliwa atashindwa kutenda haki kwa wananchi tutamuondoa hatuta
subiri mpaka miaka mitano," amesema Mbowe.
Pamoja na
mambo mengine Mbowe akiongea katika eneo la Igawiro amewataka wananchi wachague
viongozi wa CHADEMA ili wawatumikie wananchi kwa kuzingatia misingi ya chama
hicho inayojengwa katika msingi wa haki.

0 Maoni