BOT yawafungia watoa mikopo kidigitali 18

 

Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imezifungia taasisi fedha 18 zinazotoa huduma ya mikopo kidigitali kutokana na kutoa huduma hiyo bila ya kuwa na leseni pamoja na idhini kutoka BoT.

Taarifa iliyotolewa leo na Gavana wa BoT Emmanuel Tutuba imesema wameyafungia majukwa ya Programu Tumizi (Application) ya taasisi hizo zilizokiuka mwongozo kwa watoa huduma ndogo za Fedha Daraja la Pili.

Benki Kuu ya Tanzania inashirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kuzifungia programu hizi ili kuepusha umma kutumia huduma za fedha zisizokuwa na vibali vya mamlaka husika, imesema taarifa hiyo.




Chapisha Maoni

0 Maoni