Bodaboda amchoma moto mwanafunzi kisa Sh 10,000

 

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Juma Afyusisye (38) Dereva Bodaboda, Mkazi wa Iwambi Jijini Mbeya kwa tuhuma za kumjeruhi sehemu mbalimbali za mwili nwanafunzi wa kiume wa Darasa la Pili wa Shule ya Msingi Iwambi Mkazi wa Iwambi kwa kumchoma moto.

Kamanda wa Polisi Mbeya SACP Benjamin Kuzaga amesema tukio hilo limetokea Novemba 05, 2024 maeneo ya Iwambi Jijini Mbeya, ambapo inadaiwa kuwa mwanafunzi huyo kutumia shilingi 10,000/=  ya Dereva wa Bodaboda huyo.

Akisimulia tukio hilo Kamanda Kuzaga amesema Dereva wa Bodaboda alimpatia mwanafunzi huyo shilingi 10,000/ na kumuagiza aende dukani kumnunulia maandazi ya shilingi elfu 5,000/= lakini aliitumia pesa yote kwa matumizi yake binafsi.

Baada ya mwanafunzi huyo kuzitumia fedha hizo alirudi bila pesa na ndipo Dereva Juma alijichukulia sheria mkononi kwa kummwagia mafuta ya Petroli kwenye shati alilovaa na kisha kuwasha kiberiti na kumsababishia majera hasehemu mbalimbali za mwili wake.

Mwanafunzi huyo amelazwa katika Hospitali Teule ya Ifisi katika Mji Mdogo wa Mbalizi akiendelea kupatiwa matibabu.

Chapisha Maoni

0 Maoni