Binti wa miaka 9 abakwa na kuuawa kikatili kisa pipi

 

Mwanaume mmoja aitwaye Jackson maarufu kama mjomba anasakwa na Jeshi la Polisi mkoa wa Mwanza kwa tuhuma za mauaji ya binti mwenye umri wa miaka tisa aitwaye Tatu Khamis Daniel anayedaiwa kuuawa kwa kukabwa shingoni kisha kubakwa na mwili wake kutelekezwa kwenye jengo ambalo halijakamilika.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Wilbroad Mutafungwa amesema tukio hilo limetokea mnamo tarehe tatu ya mwezi huu majira ya saa mbili usiku wakati Binti huyo Tatu akiwa anacheza na wenzake ndipo akatokea Jackson maarufu kama mjomba ambae rafiki wa baba wa binti huyo, akamchukua kwa ahadi ya kwenda naye dukani kumnunulia pipi ndipo akatoweka nae kusikojulikana.

Kamanda Mutafungwa amesema hadi ilipofika kesho yake siku ya tarehe nne ya mwezi huu majira ya saa kumi na mbili na nusu katika Kijiji cha Nabweko wilayani Ukerewe ulipoonekana mwili uliokuwa umetelekezwa kwenye jengo ambalo halijakamilika kujengwa na kutambulika kuwa ni mwili wa binti huyo Tatu Khamis Daniel.

Aidha, Kamanda Mutafungwa amesema mara baada ya mwili wa binti huyo kufanyiwa uchunguzi ulibainika aliuawa kwa kukabwa shingoni kisha kubakwa na kwamba mwili huo umekabidhiwa kwa ndugu zake kwa ajili ya mazishi.

Chapisha Maoni

0 Maoni