Basi laigonga treni ya mizigo na kujeruhi abiria 14

 

Shirika la Reli Tanzania (TRC) limesema kuwa kumetokea ajali ya basi la abiria lililoigonga treni ya mizigo namba Y611 iliyokuwa ikitokea Kigoma na kusababisha mabehewa 30 kuanguka, ambapo pia katika ajali hiyo abiria 14 wamejeruhiwa hakuna vifo.

Taarifa iliyotolewa leo na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano cha TRC, Fredy Mwanjala imesema kuwa ajali hiyo imetokea usiku wa kumkia leo, ambapo dereva wa basi hilo alilipita basi lingine lililokuwa limesimama kuipisha treni na kuigonga treni.



Chapisha Maoni

0 Maoni