Askari 92 wanaojihusisha na uvuvi wahitimu mafunzo

 

Askari wanajamii 92 kutoka Tanga, Katavi, Kigoma na Rukwa wamehitimu mafunzo ya kozi fupi katika Taasisi ya Taaluma ya Wanyamapori Pasiansi (PWTI).

Mafunzo haya yamewajengea uwezo na umahiri askari hao wa vijiji vinavyojishughulisha na uvuvi na uendelezaji misitu. Mafunzo haya yalianza tarehe 22-08-24 hadi  01-11-24.

Mahafali haya ya kozi fupi ilijumuisha askari wanajamii 42: Village Fisheries Scout (VFS) waliofadhiliwa na Jane Goodall Institute na askari wanajamii hifadhi za misitu 50: Village Forest Monitors (VFM) waliofadhiliwa na Shirika la chakula duniani kupitia mradi wa Fish4ACP-FAO Tanzania.

Chapisha Maoni

0 Maoni