Uwekezaji zaidi kiwanda cha Saruji Mbeya Cement

 

Serikali kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina na Kampuni ya AMSONS Group ya Uswisi wameingia makubaliano ya kuwekeza dola milioni 300 (zaidi ya shilingi bilioni 800) katika upanuzi wa kiwanda cha Saruji cha Mbeya Cement na kuanzisha kiwanda kipya cha saruji Tanga.

Mbeya Cement, imetangaza kuongeza uwekezaji kwenye kiwanda hicho kwa kufunga mtambo mkubwa utakaowezea kuzalisha malighafi (clinker) za kutengeneza saruji tani 5,000 kwa siku kutoka tani 1,000 inazozalishwa sasa.

Hayo yamesemwa jijini Dar es Salaam leo Oktoba 15, 2024, na Msajili wa Hazina, Bw. Nehemia Mchechu akiwa pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Amsons Group, Bw. Edha Nahdi.

Sambamba na uwekezaji huo, Serikali kwa kushirikiana na mbia huyo, Amsons Group, pia wataanzisha kiwanda kingine cha saruji mkoani Tanga, kitakachokuwa na uwezo wa kuzalisha malighafi (clinker) tani 5,000 kwa siku.

“Kwa hiyo maamuzi ambayo sisi kama wanahisa tumeyafanya ni kwenda kuongeza upanjuzi na kujenga kiwanda kipya na hivyo kuonegza uzalishaji wetu kutoka tani 1,000 za sasa na kufikia tani 10,000 za clinker kwa siku,” amefafanua Bw. Mchechu.

Naye Mkurugenzi wa Fedha Mbeya Cement, Bw. Ahmed Mhada, amesema kukamilika kwa miradi hiyo kutapelekea uzalishaji wa saruji kufikia tani milioni 4.2 kwa mwaka.

Chapisha Maoni

0 Maoni